Rais
 wa Tanzania Dkt. John Magufuli amesema Serikali imetenga Shilingi 
Bilioni 483 kwa mwaka huu kwa ajili ya mikopo ya elimu ya juu ambapo 
wanafunzi zaidi ya 118,000 watanufaika.
Akizungumza
 katika uwekaji wa jiwe la msingi la hostel za Chuo Kikuu cha Dar es 
Salaam leo, Rais Magufuli amesema miongoni mwa hao watakaonufaika, 
wanafunzi 93,000 ni wanaoendelea na masomo na wanafunzi takribani 25,000
 ni watakaoanza masomo mwaka huu huku akiweka bayana kuwa mikopo hiyo 
itatolewa kwa wanafunzi ambao wanatoka kwenye familia masikini.
Rais
 Magufuli ameiagiza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kurekebisha 
dosari zilizopo katika mfumo wa utoaji wa mikopo ikiwa ni pamoja na 
upangaji mbaya wa wanafunzi katika vyuo, kutoa mikopo kwa upendeleo, 
kutozingatia sifa za mkopaji, kutoa mikopo hewa na kufungua vyuo kabla 
ya mikopo ya wanafunzi kutolewa na pia amewaonya wanafunzi kujiepusha na
 vitendo visivyofaa wakati Serikali inarekebisha dosari hizo.
"Na
 ndio maana wakati mwingine na wabaya wanapitia humo humo, mara fanye 
hivi fanyeni vile, wakati wanajua kuwa mkifanya yasiyofaa Serikali 
itawafukuza tu ili mkafanyie mambo yenu huko. 
"Kwa
 sababu huwezi kuwa unahangaika kutafuta fedha za kuwapa mikopo, wakati 
huo huo unahitaji kujenga reli, wakati huo huo unahitaji kujenga 
barabara, wakati huo huo unahitaji kulipa mishahara, wakati huo huo 
unahitaji kutoa elimu bure, wakati huo huo Karagwe kuna njaa, wakati huo
 huo watu wanahitaji dawa hospitali, halafu watu wengine wanataka 
kukuendesha kana kwamba hela unayokusanya ni kwa ajili yao tu, ni lazima
 tuelewane na mimi ninataka kuwaeleza kwa dhati lazima twende katika 
njia iliyonyooka, ni bora uwe Rais usiye maarufu lakini utimize 
uliyoyaahidi, asitokee mtu wa kukuendesha, ninajua mmenielewa" amesisitiza Dkt. Magufuli.
Dkt.
 Magufuli ameiagiza Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) kujipanga 
vizuri kukusanya marejesho ya mikopo kwa wote waliokopeshwa na bodi hiyo
 ambapo mpaka sasa bodi inadai takribani Shilingi Trilioni 2.6.
 
 

 
 
 
 
 
0 Comments
on