Kali zaidi imetokea hivi karibuni baada ya kugundulika ya kuwa vijana
wameendelea zaidi kiteknolojia katika kuhakikisha wanafanikiwa katika
kuibia kwa kutengeneza miwani ambayo inarekodi na kutuma picha hizo kwa
mwingine. Hii ni katika mtihani maarufu zaidi ujulikanao kwa jina la
Gaokao ambao unaweza kuufananisha na ule wa kuhitimu kidato cha sita kwa
hapa bongo. Ukaguzi wa wanafunzi kuingia eneo la kufanya mitihani
katika gaokao imebidi nao uwe wa kiteknolojia ya juu, na hivyo imekuwa
kama vile mwanafunzi anapita uwanja wa ndege.
![]() |
Afisa Usalama akionesha Miwani aliyokamatwa nayo mwanafunziHivi kijana wa kibongo akipata vifaa hivi si atafaulu mitihani yote hapa bongo, au wewe unaonaje? |

Kila kipindi cha mitihani walimu na hata baadhi ya shule zinatumia
polisi katika kuhaha na kusaidia katika kugundua njia zitumiwazo na
wanafunzi hao. Inasemakana ugumu wa mitihani yao pamoja na kuwa na mfumo
unafanana wa nchi kama Tanzania wa kwamba mtihani wa mwisho kubeba
miaka yote ya mtu aliyotumia shuleni unachangia katika kukuza tabia hii.

0 Comments
on