MBUNGE wa Mwibara, Kangi Lugora (CCM) amewaonya baadhi ya mawaziri kutompotosha Rais John Magufuli kuwa fedha zimepotea, kutokana na baadhi ya watu kuficha majumbani kwenye magodoro wakati hiyo si sababu.
Sambamba
 na hilo, amewaonya wabunge wa upinzani, kuacha kuwatumia vibaya 
wananchi na kuwachonganisha na Rais wao, baada ya kuona wamebanwa kulipa
 kodi.
Mbunge
 huyo alitoa onyo hilo jana wakati akichangia Mapendekezo ya Mpango wa 
Maendeleo wa Taifa kwa mwaka 2017/2018 na Mwongozo wa kuandaa mpango wa 
bajeti ya serikali kwa mwaka 2017/2018 uliowasilishwa juzi na Waziri wa 
Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango.
“Nyinyi
 mawaziri ni abiria na mmekaa siti za mbele kwenye gari analoendesha 
Rais Magufuli msimkimbize, baadhi yenu msimpotoshe rais yeye si mchumi 
mtamletea matatizo mbeleni, pesa zimepotea si kwa sababu zimefichwa 
kwenye magodoro ila zimepotea kwa sababu pesa zote zimewekwa Benki Kuu 
ya Tanzania (BoT), zitoeni pesa hizo ziende kwenye mabenki,” alisema.
Alisema Bunge limepoteza mwelekeo, limekuwa la kulialia na kumlaumu Rais Magufuli kwa sababu amebana wakwepa kodi na kufafanua “Rais
 aliliomba Bunge hili limsaidie kutumbua majibu, tumsaidie mipango ya 
serikali iweze kutekelezeka ili kujenga nchi yetu, najua Rais ana nia 
njema na nchi, Hapa Kazi Tu inawafanya wafanyabiashara waliozoea kukwepa
 kodi wamebanwa sasa wanalia biashara imekufa, watumishi waliozoea posho
 za hapa na pale, kusafiri wamebanwa, wabunge tuliozoea kula andazi la 
inchi 18 sasa tunakula la sentimita mbili, kwenye kamati tumebanwa 
posho, tunalialia kisa tumeshikwa pabaya na kuwaingiza wananchi wanyonge
 eti hawana pesa.
"Kiongozi
 wa Upinzani, Freeman Mbowe umepewa gari na serikali na mafuta 
unawekewa, yamejaa kwenye gari, kiyoyozi kipo saa 24 unasema serikali 
imefilisika huku unawachonganisha wananchi na Rais wao, unawatumia 
vibaya wananchi, Msigwa kama Mchungaji (Peter, Mbunge wa Iringa Mjini) 
tumia taaluma yako kuwashauri wenzako wawe kwenye safari hii... Rais 
Magufuli anatupeleka Kaanani kuishi maisha mazuri, ametupandisha basi 
kutupeleka nchi ya ahadi.
"Nashauri
 anapoendesha gari ajue kuna matuta, akiendesha vibaya Watanzania 
atatuangusha, kuna zebra na wanafunzi wanavuka, akiona spidi iko 50 
apunguze mwendo... na nyinyi mawaziri mmekaa siti za mbele za gari la 
Rais, msimpotoshe”, alifafanua.
Mbunge
 wa Mtera, Livingstone Lusinde(CCM) alisema ni lazima uchumi unapokua, 
uoneshe kwenye maisha ya wananchi wa vijijini ; na si kuonesha ujuaji wa
 pointi kwenye makaratasi.
Alisema “Upinzani
 msizunguke kusema serikali imefilisika, semeni ukweli, Mbowe 
umefilisika, umeshindwa kulipa madeni, serikali haijafilisika, inalipa 
mishahara, inalipa madeni yake”.
Naye
 Mbunge wa Bunda Mjini, Esther Bulaya (Chadema) alisema kila sehemu kuna
 njaa, mtaani wananchi wanalia hakuna pesa na hata wabunge wamepauka kwa
 kukosa fedha.


0 Comments
on