Rais
 wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein amesema serikali ipo madhubuti 
katika kupembua misaada ambayo wahisani mbalimbali wapo tayari na katika
 misaada ambayo itakuwa na masharti magumu kwa sasa serikali haipo 
tayari kuipokea kwa manufaa ya wananchi.
Dkt. Shein aliyasema
 hayo juzi  katika sherehe za kilele cha mbio za Mwenge zilizofanyika 
kitaifa katika mkoa wa Simiyu na kuhudhuriwa na viongozi wa serikali na 
taasisi binafsi pamoja na mamia ya wananchi pamoja na watoto wa halaiki 
waliopamba shughuli hiyo.
“Serikali
 kwa sasa tumejipanga vizuri hatutakubali misaada yenye masharti magumu 
na wahisani ambao wanataka kufanya hivyo wakae na misaada yao 
tutajitegemea wenyewe” Alisema Dkt. Shein.
Aidha Rais Dkt. Shein aliwataka
 watanzania kuendelea kuiunga mkono serikali kwa kuwa imedhamiria 
kufanya kazi kwa juhudi zote na kusema kwamba ambao wamezoea kuchukua 
rushwa ni bora waache kwa kuwa serikali haitawavumilia.
Mbio za Mwenge mwaka huu zilifikia
 tamati baada ya kukimbizwa katika mikoa 31, halmashauri 179 na siku 179
 ambapo zimezindua miradi 1,387 yenye thamani ya shilingi bilioni 498.8.
Mbio za Mwenge wa Uhuru mwakani zitazinduliwa mkoani Katavi na kuzimwa mkoani Mjini Magharibi visiwani Zanzibar.

0 Comments
on