Header Ads Widget

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 81 & 82 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )


MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA
Nikamfwata Sheila na kumkumbatia kwa furaha, huku nikimzungusha zungusha hewani na kumsimamisha chini, huku nikimbusu busu mdomoni mwake"
"Ngoja kwanza, baby nahitaji unijibu swali langu?"
"Uliza tu mke wangu nitakujibu haraka haraka"
Nilizungumza kwa furaha, kwa huku nikilisubiria kwa hamu swali ka mke wangu mtarajiwa Sheila
"PHIDAYA NI NANI YAKO?"
"Eheeee!"
"Hujanisikia nirudie au?"
Sheila alizumgumza, huku akinitazama kwa sura iliyo anza kujikunja kwa hasira kali.
 
ENDELEA
"Ohhh baby, huu sio muda muafaka wa kulizungumzia hilo, tuzungumze juu ya harusi yetu."
"Eddy nahitaji kulijua hilo, nililo kuuliza"
"Sheila unanipenda?"
 "Ndio, ninakupenda ndio maana nilikaa, bila ya kuwa na mwanaume nikikusubiria wewe"
"Ok ninakuomba tuachane na hiyo mada, kinacho paswa ni....."
"Nikujua Phidaya ni nani kwako"
Sheila alizungumza huku akiwa ame itumbulia mimacho, kwa mbali machozi yakianza kumlenga lenga. Kitu kilicho anza kunichanfanya ni namna gani amemjua Phidaya.
"Sipo katika wakati mzuri wa kulizungumzia hilo swala sasa hivi, ninakuomba tuliache"
"Eddy, Eddy, Eddy"
Sheila alizungumza, huku aking'ata meno yake, kwahasira huku machozi yakimtiririka mashavuni mwake.
Akaitoa simu yangu kwenye kipochi chake, akafungua fungua baadhi ya mafaili, na kunigeuzia kwangu. 
 
"Hii ni nini?"
Nikaiona picha ya Phidaya, akiwa na mtoto anaye fanana na mimi, ambaye John, alinibia anaitwa Junio
"Eddy kwa nini, hukua mkweli kwangu, kwa nini uliamua kuzaa na mwanamke mwengine wakati unatambua mimi nipo?"
Sheila alizungumza huku akiwa ameishika simu yangu, na kunisogezea karibu na uso wangu ili nimuone mtoto huyo, ambaye kila kitu amefanana na mimi. Hata mama akimuona hata kua na haja ya kuuliza huyu ni mtoto wa nani.
Nikaikwapua simu yangu, kutoka mkononi mwa Sheila, na kukaa kitandani huku nikiendelea kumtazama mwanangu huyu mwenye mvuto wa kila aina.
"Eddy, ni kosa gani nilikufanyia lakini, hadi ukaamua kunisaliti ehee?"
 
"Au kwasababu mimi ni muafrika, ukaona ukazad na huyo muarabu?"
"Au sikua mwanamke sahahi kwenye maisha yako si ndio?"
Sheila alizungumza huku akiendelea kulia kwa uchungu, huku akinitazama usoni mwangu. Kwa upande mmoja, nifaraja kumuona mwanangu japo kwa picha ila kwa upanfe mwengine imeanza kuniletea uchungu kwani sikuhitaji mtu yoyote atambue nina mtoto, hadi nitakapo amua mimi kufanya hivyo.
"Eddy si ninazungumza na wewe, lakini?"
"Ninakuomba unyamaze"
"Eddy siwezi kunyamaza, dhamani yangu mimi ipo wapi?"
"Sheila funga bakuli lako, unataka dhamani gani zaidi ya mimi kukuoa wewe, au unataka nimuue huyu mtoto si ndio?"
Nilizumgumza kwa kufoka huku nikimtazama Sheila, aliye anza kurudi nyuma baada mimi kunyanyuka kitandani kwa kasi. Sheila alianza kutetemeka, baada ya kugundua nimekasirika, sana. 
 
"Hii ishu ibaki kuwa mimi na wewe, sihitaji mama atambue sawa?"
"Kwa nini, hutaki ajue?"
"Hilo sio ombi, bali ni amri"
Nilizungumza na kutoka nje, kwenda sehemu ya kupumzikia, ambapo kuna baa kubwa tuu
"Nikusaidi nini?"
Dada muhudumu, alizungumza huku akinitazama machoni
"Una pombe kali?"
"Aina gani?"
"Nipe yoyote, ili mradi iwe pombe kali"
"Nusu glasi, au glasi nzima?"
"Lete mzinga mzima"
Dada huyu akanitazama mara mbili mbili, usoni na kuondoka.
 
"Hii picha ameitoa wapi huyu mwanamke?"
Nilijiuliza huku nikiendelea kuitazama picha iliyopo kwenye simu yangu. Nikapata wazo la kuingia kwenye mtandao wa Whatsappp, ila sikuona picha yoyote iliyo ingia kupitia mtandao huo. Nikaingia Viber ila sikuona chochote.
Muhudumu akaweka mzinga wa pombe kali mezani
"Usiniwekee glasi wewe nenda nayo"
Muhudumu akaondoka
"Wewe dada, ni bei gani?"
"Huo ni elfu semanini"
Nikatoa walet mfukoni na kutoa noti kumi za shilingi elfu kumi, nikamakabidhi muhudumu, akanipa asante na kuondoka. Nikaanza kufakamia mafumba ya pombe, iliyo ngumu kumeza kooni mwangu, ila muda mwengine, ikanilazimu kufumba macho ninapo imeza.
 Nikiwa kwenye dimbwi la mawazo, mlio wa simu, yangu ukanistua. Sikujua ni namba gani inayo piga kwa haraka nikaipokea na kuiweka sikioni
 
"Eddy umeoa?"
Nisauti ya Phidaya, ilisikika upande wa pili wa simu, nikajikuta nikipatwa na kigugumizi cha kulijibu swali hilo, baada ya Sheila kukaa kwenye kiti cha karibu yangu.
"Ngoja nitakupigia"
Nikakata simu, na kumtazama Sheila aliye kaa mbele yangu.
"Eddy umeanza lini kunywa?"
"Kwani vipi?"
"Nimekuuliza tuu"
"Ninakuja"
Nikanyanyuka na kumuacha Sheila peke yake mezani, nikaingia chooni na kuipiga namba aliyo ipiga Phidaya, ikaita kwa muda ikapokelewa
"Wewe nani?"
Nilisikia sauti ya mtoto ikizungumza, nikakaa kimya kusikilizia
"Mama kuna mtu amepiga simu yako, hazungumzi"
Mtoto huyo niliye amini kwamba ni Junio nilimsikia akizungumza
"Haloo"
Nikaisikia sauti ya Phidaya akizungunza
 
"Yaa ni mimi Eddy"
"Najua hilo"
"Sawa, namba yangu umeitoa wapi?"
"Hilo sio jukumu lako, ila kitubalicho kifanya huyo mwanamke wako sihakipenda"
"Amefanya kitu gani?"
"Ameniita mimi malaya, changudoa ninajipendekeza kwako, ila kitu ambacho nitakifanya hato kuja kusahau"
Nikajikuta nikishusha pumzi huku nikifikiria nikipi nizungumze.
"Ila Eddy sina haja ya kukuambia ni wapi tulipo toka, kama kukuua mimi ningekua nimesha kuua nikiwa na kuimbe chako tumboni mwangu"
"Niliweza kuvumililia kwa kila jambo, ili mradi nisikupotezee wewe. Mimi na mwanangu tunaishi kama watumwa, tunaishi maisha ya shida ya kutanga tanga. Hatuna pakuishi, hatuna pa kula kwa ajili yako."
 
"Nimetoroka kwa shida mikononi mwa John, hadi sasa hivi nimekua mwanamke wa kuishi kitumwa kwa ajili yako, hembu fikiria yote niliyo yafanya kwako kuanzia siku ulipo kua hospitalini, hadi siku najifungua mwanao mbele ya macho yako, tena kwa kudhalilika mbele ya watu wengi, ila sikujali hilo nilifanya kwasababu ya kukupenda."
Maneno ya Phidaya yakaanza kunitoa machozi taratibu huku maumivu makali yakinitawala moyoni mwangu.
"Leo hii mimi ninaitwa malaya, na huyo mwanamke wake"
"Phidaya, nakuomba unisamehe, hilo. Upo wapi?"
 
"Nipo Somalia, Mogadishu"
"Upo kwa nani?"
"Eddy nimekuambia sina sehemu ya kuishi, najishikiza kwa kufanya vibarua vya ndani. Kikubwa kinacho niumiza ni mwanangu, kuishi maisha ya shida tangu nilipo mzaa, hivi unahisi ni lini mwanao ataishi kwa furaha?"
Phidaya alizungumza pasipo kunipa nafasi yakuzungumza.
"Eddy ninakuomba usioe, tambua kua ninakupenda sana na mimi nina mwanao. Siku njema"
Phidaya akakata simu, nikajaribu kupiga simu tena haikupatikana tena.
Nikajikuta pombe iliyo anza kunichukua, ikaaanza kunititoka kichwani kauli kazaa za Phidaya zikaanza kujirudia rudia kichwani mwangu
'Eddy usioee.......Kitu nitakacho kifanya hato kuja kusahau'
Nikatoka chooni na kurudi alipo Sheila, nikakuta akiwa amejiinamia chini
"Bora umerudi, mama anataka turudi Dar kesho"
"Poa, twende tukalale"
 
******
Safari nzima yakurudi Dar es salaam, sikuwa na raha, kila nuda nikajikuta nikimkumbuka Phidaya na mwanangu. Hadi tunafika uwanja wa ndege wa J.K NYERERE, sikuwa na raha kabisa moyoni mwangu japo kila muda nilitabasamu usoni mwangu kumfanya Sheila asielewe ni kitu gani kinacho niumiza moyoni mwangu.
 
Tukapokelewa na mama, pamoja na wapambe wake, safari ya mwenda kwenye makazi mapya ya mama ikaanza. Kutokana tunatembea kwa mfumo wa msafara ulio ongozea na gari ya polisi, haikutuchukua muda mwingi barabarani. Tukafika nyumbani na kukuta wana ndugu ambao kipindi cha nyuma sikuwahi kuwaona. Nikatambulishwa kwao, ila sikuhitaji kuwajua sana kwani, kipindi tunamatatizo wao hawakuonekana
 
Siku zikazidi kusonga mbele, huku maombi yangu yakimuomba Mungu siku ya ndoa yangu isifike kwani ninahisi itakua ngumu sana. Roho moja, ikawa inahitaji nimuoe Sheila, huku rohi nyingine, ikikataa kabisa kumuoa Sheila, ikinishawishi niende Somalia, kuitafuta famili yangu
'Baba mwerevu ni hule anayekufa akipigania, familia yake'
Nimaneno yaliyo jirudia rudia kichwani mwangu. 
 
               **
Macho yangu yaliyo jaa mwangavu, wakutizama kila pande ya kanisa, yaliendelea kufanya kazi hiyo. Nikazidi kujotahidi kumuangalia kila aliye fika kanidani hapa kuishuhudia ndoa yangu. Sheila aliye pambaa vizuri, anatabasamu kila muda nilimtazama usoni mwake.
Mchungaji, akaniba nizitoe pete kwa ajilo ya kuziombea, nilafanya hivyo na kumkabidhi
 Akaziombea na kunikabidhi pete moja kwa ajili yakumvisha Sheila, nikamtazama mama yangu aliye valia nguo za dhamani.Akanikonyeza akiniashiria niweze kumvisha Sheila. Ukimya kanisani pote ukatawala, kila mmoja akinisubiria kufanya hilo. Vishindo vya viatu aina ya kokoko, vikaanza kusikika kutokea nyuma, ulipo mlango wa kanisa.
 
Ikatulazimu watu wote kugeuka kutazama, ninani anaye ingia kanisani. Nikajikuta nikitamani ardhi ipasuke, ili inimeze. Hakua mwengine, bali ni Phidaya aliye valia viatu vya juu, huku mkono wake wakulia ukiwa umemshika Junio, wakitembea kwa haraka kuja mbele tulipo.
Miaani nyeusi aliyo ivaa Phidaya, ikawafanya walinzi wa mama kumfwata, ili wamzuie, ila kila aliye mtazama Junio, alijikuta akisita kumgusa Phidaya, kwani we alitambua ni kitu gani kinacho endelea
"Phi....."
"Shiiiiii"
Phidaya alinizuia nisiseme chochote, akasimama hatua chache toka tulipo simama.
"Junio, yule ndio baba yako, ndio Eddy"
Sheila mwili mzima, unamtetemeka, Junio akaliga hatua kabla ya kufika nilipo 
"Junio"
Phidaya aliita na kumfanya mwanae ageuke kumtazama, nikamuona mama akinyanyuka huku akimtazama Junio kwa macho makali yaliyo jaa mshangao.
"Umemuona baba?"
"Ndio"
"Nakupenda mwanangu"
Phidaya alizungumza huku, alifungua zipu ya koti lake. Akalichanua, macho yangu yakatua kwenye bomu, alilo lifunga kwenye koti hilo, lililo bakisha sekunde tano kabla halijalipuka, Junioa akapiga hatua za haraka kwenda alipo simama mama yake, hata kabla hajamfikia, tukastuki mlipuko mkali, ulio turusha watu wote, ndani ya kanisa hili.

SORRY MADAM 82


"Eddy....Eddy"
Nikastuka, baada ya mama, kunitingisha mara kadhaa.
"Tumesha fika, tushuke."
Msafara wa gari za ulisha fika kwenye maegesho ya magari, nje ya duka kubwa la kuuza suti kutoka nchi mbalimbali duniani, hususani Italia na Markani.
Usingizi mfupi ulio nipitia kwa muda mchache, niliwa ndani ya gari, umenifanya niote ndoto iliyo anza kuniogopesha sana.
Nikamtazama mama kwa umakini, nikajiweka vizuri shati nililo vaa, nikashuka ndani ya gari.
"Vipi umaumwa?"
Mama aliniuliza huku tukiingia ndani ya hili duka, lililopo maeneo ya posta.
"Hapana"
"Sasa mbona hujachangamka, nini tatizo?"
"Nahisi ni uchovu wa usingizi"
Tukaanza kupitia suti moja baada ya nyingine, sikuwa na amani kabisa moyoni mwangu. Isitoshe zimesalia siku mbili kabla ya mimi kufunga ndoa na Sheila.
"Hii umeipenda?"
Mama alinionyesha suti moja yeñye rangi nyeupe yenye maua, mazuri.
"Yap"
Mama akanitazama usoni kwa umakini, huku akijaribu kunichunguza, akanigusa kwenye shingo na kiganja chake, ili kuona kama nina tatizo lolote, ila akakuta joto la mwili wangu lipo kawaida tu.
"Nenda ukaijaribishe basi"
Nikaingia moja ya chumba kilichopo hapa ndani ya duka. Nikajaribu suti aliyo nichagulia mama. Ikawa imenikaa vizuri mwilini mwangu.
"Mkuu hapa upo bomba"
Jamaa mmoja muuzaji alinisifia baada ya mimi jutika ndani ya chumba hichi, nikiwa nimevalia suti hiyo. Kila nilipo mtazama mama, nikawa ninakumbuka mlipuko nilio uota kanisani.
"Hapo mkeo atafurahi sana"
"Hongera kaka, umependeza sana"
Baadhi ya watu ndani ya duka, hawakusita kuniambia ukweli, wa kupendeza kwa jinsi nilivyo vaa. Mama alipo ridhia, akalipia suti hiyo, nikaivua na kurudi ndani ya gari.
'Junio umemuona babà?'
Sauti ya Phidaya, ilianza kujirudia rudia kichwani mwangu. Jambo lililo nikosesha amani kabisa moyoni mwangu.
"Mama, tunaweza tafuta sehemu tukazungumza?"
Nilimuuliza mama mara baada ya yeye kuingia ndani ya gari
"Tutazungumza nyumbani"
 
"Hayo nataka tuzungumze nje ya nyumbani"
"Dula, hembu tupitisheni hapo Serena"
Mama alumuambia fereva wake, akawasiliana na wezake waliopo kwenye gari moja ya mbele na nyingine gari moja lililopo nyuma yetu. Msafara ukabadilika kama alivyo sema mama, tukafika serena Hotel, nakupokelewa na wahudumu. Tukatafuta sehemu iliyo tulia na kaa mimi na mama, hata mlizi wake, wa kike aliamua kukaa mbali kidogo na ilipo meza yetu, asisikie tunacho kizungumza.
"Heee una lipi la kuzungumza?"
"Mama, ninaamini kwamba nilisha wahi kukukosea mimi kama mwanao wa pekee."
"Ila uliweza kunisamehee, kwani mtoto kwa mama, hua akui. Kama tunavyo sema sisi waswahili"
"Ndio mwanangu, nalitambua hilo"
"Màma, kunakitu ninahitaji nikuombe?"
"Omba tu mwanangu, usipo niomba wewe ni nani atakaye niomba mwengine"
Nikashusha pumzi tataribu, huku nikitazama chini, kwani hata ujasiri wa kumtazama mama, machoni ulinipotea gafla.
 
"Mama...."
"Mmmm"
Nikajikuta nikishusha pumzii kwa nguvu. Kila nilicho taka kukizungumza kikanipotea gafla kichwani mwanfu, nikajikuta nikibaki.
"Zungumza mbona umekaa kimya?"
"Nilitaka kukuambia kua...."
"Kua nina kupenda sana mama yangu. Upendo wangu sijawahi kuweka bayana kwako. Mama yangu wewe ni mfano mzurikwenye maisha yangu
 Hakuna mama kama wewe"
Maneno yangu, yakapelekea hadi mama kulengwa lengwa na machozi.
"Nakupenda pia mwanangu, nipo tayari kuupoteza utajiri wañgu, ila si wewe mwanangu"
"Japo wamama wengi, hawapendi kuwaomba misamaha watoto wao, ila kwangu nitofauti."
"Eddy mwanangi, ninakuomba unisamehe"
"Nikusamehe kwa kipi mama?"
 
Mama akajifuta machozi kwa kitambaa, chake. Akavichukua viganja vyangu, na kuvikutanisha kwa pamoja.
"Najua matatizo yote, yaliyo kupata chanzo ni mimi. Niliamua kuzaa na mdogo wa Gidwin kwa ajili ya....."
"No mama, hlo nilisha kusamehe, siku nyingi. Haikuwa kisa lako kufanya vile, pia nashukuru kwakuzaa na baba yangu, ila si godwin"
Mama akakaa kimya, hakutarajia kama nitazungumza kitu kama hicho. Kabla hatujazumgumza, simu yangu ikaita, nikaitoa mfukoni na kukuta Sheila ndio anaye piga.
"Mume"
"Mmm"
"Mumefikia wapi?"
"Tupi Serena"
"Na nani upo?"
"Kwani nyumbani, nilitoka na nani?"
”Mama"
 
"Sasa inakuaje, unauliza kwamba nipo na nani?"
"Samahani mume wangu, kama nimefanya kosa"
"Poa"
"Piga picha unitumie whatsapp, nimekumis mume wangu"
"Poa"
"Jamani Eddy, mbona unanijibu kihasira, kuna kitu nimekuudhi?"
"Hujaniudhi, ngoja nitakupigia"
"Nitumie basi picha sasa hivi, ukiwa na ma.."
Nikakata simu, kabla hata Sheila hajamalizia, sentensi yake
"Mbona unamjibu mwenzako kihasira?"
"Hapana mama, yeye anataka picha ya eneo nililopo, naona ananisumbua"
"Ndio lazima akusumbue, kutoana na mimba aliyo ibeba. Na mwamke akiwa katika kipindi hicho usidhubutu kumuudhi, anaweza kuchukua maamuzi ua ajabu, baadaye ukaja kujutia"
 
"Nimekuelewa mama"
"Lete, simu yako nikupige picha umtumie"
Nikampa mama simu, akanza kunipiga picha, kadhaa
"Tayari?"
Nilimuuliza mama
"Ndio ngoja nizitazame kama, umetokelezea"
Nikajikuta nikicheka kwani, sikujua kama mama naye anayatambua maneno ya vijana, kama kutokelezea. Nikaiona sura ya mama, ikibadilika taratibu, huku mikonjo kadhaa ikiwa kwenye uso wake.
"Huyu nani?"
Mama akanionyesha picha ya Phidaya, akiwa na Junio.
"Ahaaa... huyo ni, ni, ni n......."
"Nani?"
Rafiki yangu"
Nilijibu kwa kubabaika sana, mama akanitazama kwa macho makali sana, usoni mwangu.
 
"Huyu mtoto?"
"Eheee"
"Hujanisikia vizuri au?"
Mama aliniuliza kwa sauti ya ukali, nikajikuta nikikosa cha kujibu.
"Mam..."
"Huyu ni nani kwako?"
"Mama huyo ni Junio"
"Eddy ni ujinga gani umefanya, unazaa na hawa magaidi, Unataka ulipuliwe na mabomu ehee?"
Mama alipo zungumzia swala la julipuka kwa mabomu, moyo wangu ukanza kunienda mbio, kiasi cha kumbukumbu kadhaa za ndoto niliyo iota ndani gari ikanijia kichwani mwangu, kama mkanda wa filamu.
"Eddy, laiti ungejua, binadamu ninao wachukia ni huo waarabu"
"Hivi unawaju vizuri kweli wewe?"
"Ila mama..."
 
"Edddy hakuna cha ila hapa, kwa nini hujasema, kwba una mwanamke umezaa naye?"
"Mama ninakuomba, utulize jazba, nataka nikuelezee kila kitu juu ya huyo msichana"
"Kwanza ni mtu wa nchi gani?"
"Iraque"
"Mungu wangu, Eddy mwanangu umeingia pabaya"
"Maa sio pabaya ninampenda sana huyo mwanake ni mama wa mwana....."
Kibao kikali kikatua shavuni mwangu, kitendo kilicho mganya hadi mlinzi wa mama akastuka.
"Funga bakuli lako, mbwa wewee. Habari ni hii, simtambui huyo malaya wako wa kiarabu, na wala sikitambui hicho kingurue chako.Ninaye mtambua ni Sheila tuu na mjukuu wangu ajaye."
Mama alizungumza kwa hasira, huku machozi yakimtiririka mashavuni mwake
 
"Mama, mwanamgu ni ngurue?"
"Kama ulivyo sikia"
Mama akanyanyuka, na kuanza kuondoka huku akitazama chini, ili watuwasiguñdue kwamba analia.
"Mama sinto muoa Sheilaa"
Nilizunguza kwa sauti ya juu, iliyo mfanya mana kugeuka kwa hasira na kurudi nilipo simama
"KAMA MIMI SIJAKUWEKA, TUMBONI MWAÑGU MIEZI TISA, HUTO MUOA SHEILA, ILA KAMA NILIKUZA KWA UCHUNGU, BASI UTAMUOÀ SHEILA."
"HICHO KIBESI CHAKO WAPANDISHIE HAO WASICHANA WAKO, ILA SI MIMI MAMA YAKO. USIPO ANGALIA NITAMPOTEZA HUYO MBWA WAKO NA KITOTO CHAKE"
Mama alizungumza na kupiga hatua tatu mbele akanigeukia na kwaishara ya kidole chake, akaniamrisha nitangulie kwenye gari, huku yeye na mlinzi wake wakifwatia nyuma.

 ==> ITAENDELEA

Usikose kufuatilia sehemu inayofuata kupitiaDJADAM64.COM

Post a Comment

0 Comments